23/11/2025
Osimhen alisema alikuwa anamtumia pesa mara kwa mara rafiki yake wa utotoni. Siku moja, rafiki huyo alimuomba msaada wa pesa ya kuanzisha biashara, na Osimhen akamtumia €5,000 (takribani Naira milioni 8). kwa Tanzania ni sawa na (Million 14)
-- Kwa moyo wa upendo, Osimhen alimtumia €5,000. Lakini badala ya kushukuru, rafiki yake huyo alimwambia kuwa alitegemea €50,000, akidai alisoma kwenye habari na kuona Osimhen anapokea €1 million kwa wiki.
Osimhen aliumia sana. na Alisema wazi: alitamani kurudisha pesa hizo, lakini hakuweza.
Alisema €5,000 inaweza kununua jozi moja tu ya viatu Ulaya, lakini kiasi hicho ni pesa nyingi sana nchini Nigeria 🇳🇬
-- Alisisitiza kwamba hakuna mtu aliyemtumia hata dola moja kabla hajakwenda Ulaya. Alifanya jitihada kubwa mchana na usiku, ikiwemo kuuza maji ya chupa barabarani nchini kwao Nigeria, ili kufadhili ndoto zake za mpira.
Funzo:
Si kila aliyekuwa karibu na safari yako ya chini anastahili kiti kwenye meza ya mafanikio yako.Wengine hawana shida na hali yako, wana shida na kutopata wanachodhani unawadai 🙄
စာတို