mpishi_mzoefu

mpishi_mzoefu Nakufundisha mapishi ya Biashara na Nyumbani
Follow Ujifunze upate faida

30/04/2026

Kuku vuruga

Mahitaji

Kuku

Hoho

Caroti

Kitunguu maji

Kitunguu swaumu

Tangawizi

Chunvi

Viazi

Jinsi ya kuandaa

Chukua kuku muoshe vizuri,weka kwenye chombo safi kisha Chukua kitunguu swaumu na tangaziwizi kiasi saga,

Chukua mchanganyiko uliousaga wa kitunguu swaum na tangaziwizi kisha changanya na kuku pamoja na chunvi kiasi na Mafuta kidogo(Marination) Acha Dk 15,

Baada ya dakika 15 mkaange kuku,Akakaule kiasi,Kisha chukua zile hoho,caroti na kitunguu vikate kwa urefu

Weka sufuria jikoni kisha weka Mafuta kiasi,weka kitunguu swaum kiasi,baaada ya hapo weka mbogamboga ulizoandaa Yaani,Hoho caroti na kitunguu

Pika hadi mboga zilainike kiasi alafu weka kuku,ongeza nyanya kidogo ya kusaga, k**a huna unaweza kutumia tomato sauce,weka ndimu kiasi na soy sauce(k**a unayo sio lazima)

Baada ya hatua hizo menya viazi Kisha vioshe vizuri,vikate na uvikaange hadi vikauke,

Changanya viazi pamoja na yule kuku uliye mpika,Kisha pakua,Tayari kwa kula

https://mpishimzoefu.blogspot.com/2025/04/jinsi-ya-kupika-kuku-wa-kuvuruga-na.html

30/04/2026

Pilau rahisi halina mambo mengi fuatana nami uweze kupika mwenyewe nyumbani kwako,

Mahitaji

1.Mchele Kg 3

2.Mafuta ½Ltr

3.Vitunguu maji ½ kg

4.Kitunguu swaum ¼kikombe

5.Pilau masala 3

6.Nyama 1kg

7.Viazi ½

8.Binzari nyembamba 5

9.Ajinamoto

10.Chunvi

Mahitaji, ndo hayo k**a nilivyokutangulia kusema,halina mambo mengi ila mitamu balaa,

Jinsi ya kuandaa

1.Chukua sufuria weka jikoni,Kisha weka Mafuta,Yakipata moto weka vitunguu

Kisha pika kwa kukoroga hadi viwe brown(Visiungue pilau litakuwa chungu)

2.Weka maji kikombe kimoja Ili vitunguu vibaki na rangi ya brown,visiendelee kukaangika vikaungua,Kisha weka kitunguu swaumu endelea kukoroga Kisha weka pilau Masala

3.Weka nyama,viazi koroga kisha ongeza chunvi na ajinamoto,kisha osha mchele na kuuweka endelea kukoroga

NB:Zingatia usioshe mchele au kuuloweka mapema,Mchele uoshe unapokuwa umeshafikia hatua ya kuuweka kwenye viungo Ili usinywe maji mengi Unaweza kukusumbua kwenye kupika ukatoa bokoboko.

4.Baada ya kuweka mchele weka mchuzi uliochemshia nyama uwe wa moto,Kisha koroga hadi uone pilau limekuwa zito mfano wa tope,Alafu ondoa jikoni weka pembeni

5.Ondoa mkaa jikoni,bakisha kidogo sana alafu funika pilau vizuri na foili na mfuniko kwa juu Kisha weka mkaa juu subiri

Baada ya dk30 funua alafu weka Binzari nyembamba Kisha geuza pilau,Lifunike tena kwa dakika 10.Baada ya hizo dakika pilau litakuwa tayari.

https://mpishimzoefu.blogspot.com/2025/03/jinsi-ya-kupika-pilau.html

30/04/2026

Kwa wale ambao wanaandaa vyakula vya sherehe mbalimbali, potato wedges zinaweza kuwa k**a dish mojawapo,

Pia Unaweza kufanya k**a mbadala wa chips Ili kupunguza gharama Kwa maana kwa pishi hili mtu atatumia Viazi vichache ukilinganisha na chips.

Mahitaji:

1.Viazi mbatata(Viazi vya chips)

2.Coriander(giligilani/Cotmil)

3.Kitunguu,Hoho,Caroti,Mafuta na chunvi

4.Vinegar, Soy sauce

Jinsi ya kuandaa

1.Chukua Viazi vikubwa vimenye kisha vikate mara nne k**a inavyoonekana kwenye picha, Yaani kiazi kimoja kitoke vipande vinne.

2.Kaanga Viazi kwakutumia Mafuta mengi(Yaani Deep fry) geuza kwa kutumia mwiko na sio kijiko Ili visivunjike.

✓Hakikisha vinakauka vizuri.

Kisha chukua hoho nusu Caroti nusu na kitunguu nusu(Inategemea unaandaa kwa wingi kiasi gani).

Picha:

3.Mimi nimekuandikia kwa makadirio tu).Kisha saga kwenye blendar kwa kuweka Mafuta kiasi soy sauce kiasi na vinegar,na chunvi kiasi.

4.Kisha huo mchanganyiko uliousaga,Weka jikoni kwenye chombo Kisha pika hadi ikauke uwe nzito kiasi(Huo mchanganyiko ukishapikwa unaitwa Sauce).

5.Chukua Coriander zikatekate vipande vigogo(Chop) alafu fuata hatua hizi hapa chini.

6.Utachukua Viazi ulivyokaanga,Utaweka kwenye chomba safi kisha utakuchua kijiko utachota Sauce utamimina juu ya Viazi

7. Kisha utaanza kuchanganya kwa kurusha rusha(mfano k**a unavyopepeta Michele).

8.Utaona Viazi vimebadilika rangi Kisha utachanganya kwa kuongeza coriander.

Baada ya kufuata hatua hizo utakuwa umemaliza kuandaa POTATO WEDGES 🥔

https://mpishimzoefu.blogspot.com/2025/03/jinsi-ya-kupika-potato-wedgesviazi-vya.html

30/04/2026

Mahitaji.
Unga wa Ngano 1Kg
Sukari 1 Kijiko cha chakula
Chunvi 1 Kijiko cha Chakula
Maji ya uvuguvugu
Mafuta ya kula

NJIA.

SIRI. Hii hapa siri ya kupika chapati laini,Nikwamba Weka mafuta mwishoni kabisa yaani usiweke mafuta kwenye unga kabla ya kuweka maji.

Chukua chombo safi,Weka unga wa ngano,Kisha weka chunvi na sukari Changanya alafu weka maji ya Uvuguvugu.Endelea kuongeza maji kidogo kidogo ili maji yasizidi.

Kanda kwa muda kisha weka Mafuta.Kanda k**a dk 10,Kisha funika kwa muda wa dk 20

Baada ya hapo kata Saizi ya chapati unazohitaji Alafu sukuma na kuchoma.

Wakati wa kuchomachapati,Kwenye kikaango(Frying pan) Usiweke mafuta kwanza,Ila anza kuweka chapati,

Alafu ikianza kubabuka geuza na weka mafuta upande ule uliobabuka,Kisha fanya hivyo pia kwa upande wa Pili.Usiweka mafuta kabla chapati haijababuka itatoka vibaya.

Imeandaliwa na:Mpishi Mzoefu

Ukiona posti hii,Ona K**a umekutana na Mimi Nipigie uliza Umekwama wapi? 0765848756

Mpishi mzoefu Home of Delicious Food

https://mpishimzoefu.blogspot.com/2023/04/jinsi-ya-kupika-chapati-laini.html

30/04/2026

JINSI YA KUCHANGANYA VIUNGO KWAAJILI YA KUPIKA ROST

Rost la aina hii unaweza kulitumia kwaajili ya kuku,samaki,nyama nk lakini jambo moja na muhimu la kuzingatia ni kuhakikisha kwamba utaongeza kiungo mojawapo mf, K**a unapika samaki utaongeza fish masala,au Chicken masala k**a unapika kuku,vilenile k**a unapika Nyama basi utaongeza Beef masala

Mahitaji

Curry Powder kijiko cha chai

Chilly powder kijiko cha chai

Kitunguu swaum kijiko komoja cha chakula

Tangawizi kijiko kimoja cha chakula

Binzari manjano kijiko kimoja cha chai

Tomato paste vijiko 3 vya chakula

Galam masala kijiko kimoja cha chakula

NB,Unaweza kuongeza zaidi kipimo kutokana na wingi wa mboga unayopika

Weka viungo vyote kwenye bakuri k**a vilivyoorodheshwa kisha changanya vizuri

JINSI YA KUTUMIA

Iwapo utakuwa umeshaandaa masala yako k**a nilivyoelekeza hapo juu,Hatua itakayofuata ni kupika.

1.Chukua chombo safi weka mafuta

2.Mafuta yakipata moto weka kitunguu maji

3.weka kitunguu swaum na Tanzawizi

Pika kwa sekunde chache kisha weka Masala uliyoiandaa

Baada ya kuweka madsala unapika masala yako kwa dk 3 kisha uanaweka mboga yako k**a ni kuku au samak,Nyama nk kisha utaogeza maji kiasi na chunvi kisha utaondoa rost lako litakuwa tayari

Imeandaliwa na Chef Shedrack

Mawasiliano 0765848756

Instagram Mpishi_Mzoefu

https://mpishimzoefu.blogspot.com/2020/07/jinsi-ya-kuandaa-rost-kwaajili-ya.html

30/04/2026

Mahitaji

Unga wa ngano

Sukari

Mafuta

Amila

Tui la n**i

Njia

Chukua chombo safi weka unga na sukari kisha changanya vizuri kwa mikono,Weka mafuta ya moto kiasi k**a robo kikombe kwa unga kg 1 na endelea kuchanganya vizuri

Weka amila na endelea kuchanganya vizizuri,kisha weka N**i changanya kwa kutumia mikono,chukua maji ya uvuguvugu ongeza kwenye unga wako kisha anza kukanda.Baada ya kukanda lifunike donge lako kwa muda usiopungua Dk 20 ili liweze kuumka

Baada ya hatua hizi sukuma donge lako kisha kata saizi ya mandazi unayohitaji,na baada ya kukata saizi ya mandazi uanyohitaji,anza kukaanga[kuchoma]kwa kina kirefu cha mafuta]

NB;Mafuta hayatakiwi kuwa ya moto sana ili mandazi yaweze kuiva hadi ndani

baaada ya kumaliza kuakanga mandazi yote yatakuwa tayari kwa kuandaa

AHSANTENI!

https://mpishimzoefu.blogspot.com/2020/04/jinsi-ya-kupika-mandazi-ya-n**i.html

30/04/2026

MAHITAJI
Unga wa ngano nusu
Mayai mawili
Maziwa vijiko viwili vya chakula
Chunvi robo kijiko cha chakula
Caroti
Blueband nusu kijiko cha chakula

NJIA
Chukua chombo safi weka unga kisha weka maji ya uvuguvugu kisha changanya kwa kukoga
Weka mayai kisha endelea kukoroga kisha kwangua karoti kiasi changanya pamoja

4.Weka chunvi kiasi kisha koroga ili kupata mchanganyiko mzuri,Baada ya hapo mchanganyiko wako utakuwa tayari

5.Chukua kikombe au kijiko kikubwa chota size ya chapati unayohitaji kisha choma[kaanga]pande zote mbili,Pika hadi umalize uchanganyiko wote uliyoandaa

AHSANTENI SANA!

mpishimzoefu.blogspot.com

https://mpishimzoefu.blogspot.com/2020/04/jinsi-ya-kupika-chapati-za-maji.html

30/04/2026

Mahtaji

Nyama ya kusaga ½

Kitunguu saum

Tangawizi

Nyanya zilizosagwa

Galam masala

Njia

Chukua nyama weka kwenye chombo safi kisha weka tangawizi kiasi na kitunguu saum kiasi,weka Tangawizi kiasi kisha weka chunvi kidogo acha kwa muda Wa Dk ,30

Chukua chombo safi weka jikoni kisha weka mafuta kiasi kisha weka kitunguu

kaaga hadi iwe rangi ya brown kisha weka nyanya(zilizosagwa) kisha weka galam masala Endelea kumix pamoja kwa muda kisha acha kwa Dk 3 alafu ondoa

Tayari kwa kuandaa utapata muonekano huo hapo chini

https://mpishimzoefu.blogspot.com/2018/12/jinsi-ya-kupika-blologinize-rosti-la.html

30/04/2026

Mahtaji

Kitunguu saum

Tangawizi

Mayai

Seasord flower

Unga wa mkate

Njia

Chukua samaki sehemu ya steck osha vizuri,weka kwenye chombo safi,weka kitunguu swaum kiasi Na Tangawizi kiasi,weka mafuta kidogo (Acha kwa muda Wa Dk 30)Kisha

Chukua unga Wa ngano kiasi weka black paper( Pilipili Manga) alafu weka chunvi kiasi,Chicken masala Na Galam masala



Chukua mayai mawili yapasue weka kwenye chombo safi

Weka unga Wa mkate kwenye chombo safi

★Kumbuka samaki wako unawakata kwa urefu alafu tenganisha mifupa Na nyama ya samaki

Cchukua kipande kimoja baada ya kingine fuata hatua zifuatazo

Chovya kipande cha kwanza kwenye unga Wa ngano

Kisha chovya kwenye yai mwisho kabsa chovya kwenye unga Wa mkate .Baada ya kumaliza hatua zote hizo kwa vipande vyote vya samaki,Chukua chombo weka jikoni weka mafuta yakipata moto kaanga samaki wako hadi wawe blown baada ya hapo ondoa Tayari kwa kuandaa

https://mpishimzoefu.blogspot.com/2018/12/jinsi-ya-kupika-samaki-fillet-fish.html

20/03/2026

Comment ziwe fupifupi

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when mpishi_mzoefu posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to mpishi_mzoefu:

Share

Category