06/09/2026
Upako ni nini? Kwa ufupi sana upako ni nguvu za MUNGU,huwezi kushinda mambo ya rohoni bila kuwa na upako au nguvu za MUNGU ,watu wengi hawaelewi wanaposikia neno upako,pia watu wengi wanafikili ukiomba tu tayali MUNGU anajibu apana Kuna vigezo na hatua mbalimbali.ili uweze kupata majibu lazima uwe na nguvu za MUNGU,na nguvu za MUNGU huzipati bila utakatifu au usafi wa rohoni,baada ya hapo maombi yako hupitia michakato mbalimbali kwanza ROHO MTAKATIFU huyapangilia vizuri na baadae huyapeleka mikononi mwa Malaka wa kwanza na baadae malaika wa pili mpaka kwa MUNGU mwenyewe.
Warumi 8:26
Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Ufunuo wa Yohana 5:8
Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu.
Ufunuo wa Yohana 8:3
Na malaika mwingine akaja akasimama mbele ya madhabahu, mwenye chetezo cha dhahabu, akapewa uvumba mwingi, ili autie pamoja na maombi ya watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu, iliyo mbele ya kiti cha enzi.
Ufunuo wa Yohana 8:4
Na moshi wa ule uvumba ukapanda mbele za Mungu pamoja na maombi ya watakatifu, kutoka mkononi mwa malaika.