Tumwesige Mixed Farm

Tumwesige Mixed Farm Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Tumwesige Mixed Farm, Farm, +255714887774, Dodoma.

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KABLA HUJAANZA UFUGAJI KUKUKabla hujaanza ufugaji wa kuku, kuna mambo muhimu ambayo kila mfug...
29/03/2026

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KABLA HUJAANZA UFUGAJI KUKU

Kabla hujaanza ufugaji wa kuku, kuna mambo muhimu ambayo kila mfugaji anapaswa kuyazingatia ili kuepuka hasara na kuhakikisha biashara yako inafanikiwa:

1. Chagua aina sahihi ya kuku Je, unataka kienyeji, broiler, au improved? Kila aina ina malengo tofauti.

2. Jua soko lako Hakikisha unajua wateja wako na bei nzuri ya kuuza mayai au kuku mzima.

3. Bajeti na gharama – Andika bajeti yako kwa kina, ukijumlisha chakula, dawa, chanjo, na ujenzi wa banda.

4. Banda bora – Banda lazima liwe safi, lenye hewa nzuri, na linazuia magonjwa.

5. Vyakula na malisho mbadala – Jua jinsi ya kuchanganya vyakula na kutumia vyakula mbadala k**a Azola na Funza kupunguza gharama.

6. Chanjo na dawa za kuku – Jua ratiba ya chanjo na dawa muhimu ili kuzuia magonjwa.

7. Maji safi na usafi – Kuku wanahitaji maji safi kila wakati; usafi wa banda ni kipaumbele.

8. Ratiba ya ufugaji – Pangilia kila hatua kuanzia kununua vifaranga, lishe, chanjo, hadi mauzo.

Kumbuka: Ufugaji bila maandalizi unaleta hasara. Anza kwa maarifa, plan nzuri, na utayari wa kushughulikia changamoto.

:-Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774

:-Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774
29/03/2026

:-Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774

Homa Kali ya Matumbo (Fowl Typhoid) Ni ugonjwa wa kuku unaosababishwa na bacteria na hushambulia zaidi kuku wakubwa pia ...
08/01/2026

Homa Kali ya Matumbo (Fowl Typhoid)
Ni ugonjwa wa kuku unaosababishwa na bacteria na hushambulia zaidi kuku
wakubwa pia na vifaranga. Ugonjwa pia hushambulia aina zote za bata, kanga na ndege
wa porini.
Jinsi Ugonjwa Unavyoenea: Chanzo cha maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa
na kinyesi cha kuku wagonjwa. Panya, ndege na wanyama wengine wanaweza kueneza
ugonjwa kwa kubeba mizoga ya kuku waliokufa kwa ugonjwa na kuchafua maji na vyakula.
Maambukizi pia yanaweza kupitia katika mayai yanayototolewa na vifaranga kuathirika. Pia
mashine za kutotolea zilizochafuliwa zinaweza kuambukiza vifaranga.

Dalili
Kuku wakubwa
• Kuharisha kinyesi cha majimaji na cha rangi ya njano
• Vifo vya ghafla
• Kupauka kwa upanga na masikio kwa sababu ya kupungukiwa damu
• Manyoya hutimka, hushusha mbawa, hufumba macho na kuzubaa (kuvaa koti)

Vifaranga
• Vifaranga wanatotolewa wakiwa wamekufa au dhaifu
• Hujikusanya pamoja na kukosa hamu ya kula
• Kinyesi cha rangi ya njano na huganda kwenye manyoya ya sehemu ya kutolea haja
• Hupumua kwa haraka na kwa shida
• Vifo vingi huweza kutokea kuku wasipotibiwa

Tiba
• Yapo madawa mengi aina ya antibiotiki ambayo yanaweza kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa.
Lakini madawa haya hayawezi kumaliza kabisa ugonjwa kutoka shamban au Tumia Enrofloxacin 1 ml kwa lita 2 za maji siku 5–7, kisha wape vitamini.

Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774

🐓...Hivi Unafahamu Kwamba Ufugaji Wa Kuku Unafursa Nyingi Sana Na Kila Mfugaji Anaweza Chagua Fursa Moja Wapo Na Ikamtoa...
08/01/2026

🐓...Hivi Unafahamu Kwamba Ufugaji Wa Kuku Unafursa Nyingi Sana Na Kila Mfugaji Anaweza Chagua Fursa Moja Wapo Na Ikamtoa Kimaisha...???

❌Kuna Kundi Kubwa La Wafugaji Wanaingia Kwenye Tasinia Hii Ya Ufugaji Bila Kujua Wanahitaji Nini..??? Yaani Mtu Anaanza Ufugaji Ila Hajui Ameingia Kwenye Ufugaji Ili Apambane Na Fursa Ipi...???

🧓Wahenga Wanamsemo Wao Usemao Hivi...👇👇👇

"K**A HUJUI UNAELEKEA WAPI BASI JIANDAE KUPOTEA AU KUTUMIA NGUVU KUBWA KUFIKA UNAPOHITAJI UFIKE"

✍️Maana Yetu Ni Kwamba Kila Jambo Linahitaji Liwe Na Mipango Yaani Ufugaji Pia Unahitaji Uwe Na Malengo Mahususi Ili Pindi Unapoanza Safari Yako Ya Ufugaji Ujue Unaelekea Wapi..??? Nitumie Njia Ipi Kufika Huko Ninapotaka Kufika...??? Na Nitumie Mbinu Gani Za Kunifikisha Kwenye Malengo...???

🤔...SWALI KWAKO MFUGAJI...???🤔

👉Je...??? Wewe Msomaji Wetu Unayesoma Huu Ujumbe Muda Huu Umeona Fursa Gani Kwenye Ufugaji Wa Kuku Na Pia Tuambie Kwenye Uwanja Wa Comments Umejipanga Vipi Kufikia Hayo Malengo...???

Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774

Utunzaji wa kuku wa mayai tangu vifaranga hadi wanapoanza kutaga ni muhimu sana ili kupata uzalishaji bora. Hapa kuna ha...
08/01/2026

Utunzaji wa kuku wa mayai tangu vifaranga hadi wanapoanza kutaga ni muhimu sana ili kupata uzalishaji bora. Hapa kuna hatua za msingi za kufuata:

1. Maandalizi ya Sehemu kwa Vifaranga

Joto: Weka kifaa cha kutoa joto (brooder) ndani ya banda la vifaranga. Mwanzoni, joto linapaswa kuwa 32-35°C, kisha upunguze kwa 2-3°C kila wiki hadi vifaranga wafikishe wiki 6.
Sehemu Salama: Banda liwe na ulinzi dhidi ya wanyama hatari k**a vile paka au mbwa. Hakikisha kuwa na hewa ya kutosha bila baridi kali.
Utando wa Sakafu: Tumia utando k**a maranda au majani kavu kuweka sakafu safi na kavu.
2. Chakula na Maji

Chakula: Vifaranga wanahitaji chakula maalum kinachoitwa starter mash kwa wiki za kwanza 8. Chakula hiki kina protini nyingi (18-20%) kusaidia ukuaji.
Maji: Kuwe na maji safi na ya kutosha wakati wote. Ongeza virutubisho k**a vile vitamini na dawa za kinga mwanzoni mwa maisha yao.
3. Mwangaza

Wape vifaranga mwangaza wa masaa 22 kwa siku kwa wiki ya kwanza, kisha polepole punguza hadi masaa 14. Mwangaza huu unasaidia ukuaji bora wa mifupa na misuli.
4. Chanjo na Matibabu

Chanjo ya Newcastle: Chanjo hii inatolewa siku ya 7 baada ya kuzaliwa.
Chanjo ya Gumboro: Hii hufanyika mara mbili, siku ya 14 na 28.
Matibabu ya Minyoo: Mara kwa mara, weka dawa ya minyoo kwenye maji ya kunywa.
5. Utunzaji wa Kuku wa Umri wa Kati (Wiki 8 hadi 18)

Chakula: Badilisha chakula kutoka starter mash hadi grower mash, chenye protini ya wastani (16%).
Maji: Hakikisha wana maji safi muda wote.
Mazingira: Waweke katika mazingira yenye nafasi ya kutosha kwa kila kuku ili kuzuia msongamano.
6. Kuku Waanzao Kuweka Mayai (Wiki 18 hadi 20)

Chakula: Wape layer mash chenye virutubisho vinavyosaidia uzalishaji wa mayai, k**a kalsiamu kwa ajili ya nguvu ya magamba ya mayai.
Vifaa vya Kutagia: Hakikisha unaweka viota (nesting boxes) ili kuku watagie kwenye sehemu safi na tulivu.
Udhibiti wa Magonjwa: Endelea na mpango wa chanjo na matibabu ya minyoo kila baada ya miezi kadhaa.
7. Udhibiti wa Mazingira

Usafi: Safisha banda mara kwa mara ili kuzuia magonjwa.
Heathari ya Hali ya Hewa: Wakati wa baridi kali, hakikisha banda ni lenye joto la kutosha. Wakati wa joto kali, toa kivuli na kuhakikisha kuna uingizaji hewa wa kutosha.
Kwa kufuata hatua hizi, vifaranga wako watakua na kuwa kuku wenye afya, ambao wanatoa mayai kwa wingi na kwa ubora

Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774

Ratiba ya chanjo kwa magonjwa mbalimbali ni muhimu sana kwa wafugaji wa kuku ili kuwalinda dhidi ya magonjwa hatari amba...
08/01/2026

Ratiba ya chanjo kwa magonjwa mbalimbali ni muhimu sana kwa wafugaji wa kuku ili kuwalinda dhidi ya magonjwa hatari ambayo yanaweza kuleta hasara kubwa. Hapa ni ratiba ya chanjo inayopendekezwa kwa mfugaji wa kuku:

1. Kideli au Mdondo (Newcastle Disease)

Chanjo ya Kwanza: Siku ya 7.
Chanjo ya Pili: Siku ya 21.
Chanjo ya Tatu (Booster): Siku ya 42 (hasa kwa kuku wa mayai).
Njia ya Utoaji: Kwa njia ya matone machoni, puani, au kunywa.

2. Gumboro (Infectious Bursal Disease – IBD)

Chanjo ya Kwanza: Siku ya 10 hadi 14.
Chanjo ya Pili: Siku ya 21 hadi 28.
Njia ya Utoaji: Kunywa (inayochanganywa kwenye maji) au matone machoni.

3. Ugonjwa wa Mahepe (Marek’s Disease)

Chanjo ya Kwanza na ya Pekee: Siku ya 1 baada ya kutotolewa.
Njia ya Utoaji: Sindano ya ndani ya misuli (intradermal or subcutaneous injection).

4. Ugonjwa wa Ndui ya Kuku (Fowlpox)

Chanjo ya Kwanza: Wiki ya 6 hadi 8.
Chanjo ya Pili: Wiki ya 18 kwa kuku wa mayai.
Njia ya Utoaji: Sindano ya ndani ya ngozi (wing web stab).

5. Ugonjwa wa Mafua ya Kuku (Infectious Coryza)

Chanjo ya Kwanza: Wiki ya 6 hadi 8.
Chanjo ya Pili: Wiki ya 12 hadi 16.
Njia ya Utoaji: Sindano (subcutaneous or intramuscular injection).

6. Infectious Bronchitis (IB)

Chanjo ya Kwanza: Siku ya 1.
Chanjo ya Pili: Wiki ya 4 hadi 6.
Njia ya Utoaji: Matone machoni, puani, au kupitia maji ya kunywa.

7. Taifodi ya kuku (Fowl Typhoid)

Chanjo ya Kwanza: Wiki ya 12 hadi 16.
Njia ya Utoaji: Sindano.

8. Avian Encephalomyelitis (AE)

Chanjo ya Kwanza: Wiki ya 10 hadi 12.
Njia ya Utoaji: Matone machoni au kunywa.

Ratiba ya Chanjo kwa Kuku wa Nyama (Broiler)

Siku ya 1: Mahepe
Siku ya 7: Kideli au Mdondo
Siku ya 10-14: Gumboro
Siku ya 21: Kideli au Mdondo (Chanjo ya pili)
Siku ya 21-28: Gumboro (Chanjo ya pili)
Ratiba ya Chanjo kwa Kuku wa Mayai (Layers)

Siku ya 1: Mahepe
Siku ya 7: Kideli au Mdondo
Siku ya 10-14: Gumboro.
Siku ya 21: Kideli au Mdondo (Chanjo ya pili)
Siku ya 21-28: Gumboro (Chanjo ya pili).
Wiki ya 6-8: Ndui ya kuku, Mafua ya kuku (Coryza)
Wiki ya 12-16: Taifodi ya kuku, Infectious Bronchitis (IB), Mafua (chanjo ya pili)
Wiki ya 18: Kideli au Mdondo (Booster).
Maelezo Muhimu:

Uhifadhi wa chanjo: Chanjo zinapaswa kuhifadhiwa kwenye hali ya baridi (chini ya 8°C).
Usafi: Hakikisha maji yanayotumika katika chanjo kupitia kunywa ni safi na hayana kemikali k**a klorini.
Kufuata Maagizo: Fuata maagizo ya chanjo kutoka kwa wataalamu wa mifugo ili kuhakikisha ufanisi wa chanjo.
Kufuata ratiba hii ya chanjo itasaidia kuzuia milipuko ya magonjwa na kuongeza uzalishaji wa mifugo.

Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774

Faida za Ufugaji wa Kuku wa Asili:Chakula – nyama ya kuku na mayai hutumika k**a chakula muhimu cha wanadamu, chenye pro...
08/01/2026

Faida za Ufugaji wa Kuku wa Asili:
Chakula – nyama ya kuku na mayai hutumika k**a chakula muhimu cha wanadamu, chenye
protini.
Chanzo cha kipato – mkulima hupata fedha akiuza kuku au mayai.
Chanzo cha ajira – ufugaji wa kuku hutoa ajira kwa jamii.
Kuku hutumika kwenye shughuli za ndoa k**a vile kutoa mahari na pia ni kitoweo muhimu
katika sherehe hizo.
Gharama nafuu za kuanzisha na kuendesha mradi huu.
Ni kitoweo rahisi na chepesi kwa wageni kuliko wanyama wakubwa k**a ng’ombe au mbuzi.
Ni kitoweo kisichohitaji hifadhi, hutumika mlo mmoja au miwili na kumalizika.
Kuku na mayai hutumika kwa tiba za asili.
Jogoo hutumika k**a saa anapowika nyakati za alfajiri na majira mengine ya siku.
Hutuhabarisha iwapo kiumbe kigeni au cha hatari kwa mlio maalum wa kuashiria hatari.
Mbolea kinyesi cha kuku kinaweza kutumika katika kurutubisha mashamba ya mazao na
mabwawa ya samaki.
Kuendeleza kizazi cha kuku wa asili hapa nchini.
Soko lipo la uhakika, ukilinganisha na kuku wa kisasa kwani nyama na mayai yake hupendwa
zaidi na walaji.
Manyoya ya kuku hutumika k**a mapambo, pia huweza kutumiaka kutengenezea mito ya
kulalia na kukalia.
Shughuli za utafiti kuku wanatumika katika tafiti nyingi za baiolojia, k**a kutambua mambo ya
lishe.
Shughuli za viwandani:
Mayai yenye mbegu ya jogoo hutumika katika kutengeneza dawa za chanjo.
Magamba ya mayai yanaweza kutumika katika utengenezaji wa vyakula vya wanyama.
Kiini cha njano cha mayai kinaweza kutumika kutengeneza mafuta ya kuoshea nywele
(shampoo).
Mapungufu ya Kuku wa Asili:
Hutaga mayai madogo wastani wa gramu 47 ambapo kuku wa kisasa wastani wa gramu 55,
aidha hutaga mayai machache wastani wa mayai 60 kwa mwaka ambapo kuku wa kisasa
huweza kutaga hadi mayai 300 kwa mwaka.
Ukuaji taratibu kuku wa asili hukua taratibu kutokana na lishe duni. Kutokana na hali hiyo kuku
huchukua muda mrefu (miezi sita) kufikia uzito wa kuchinjwa (kilo 1 - 1.5). Hali hii pia hufanya
faida ya ufugaji wa kuku wa asili kuchukua muda mrefu kupatikana.
Nyama yake ni ngumu (huchukua muda mrefu kuiva) ikilinganishwa na kuku wa kisasa.

Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774

JE WAJUA...???🐓🐓🗣️Ukweli Usioujua Kuhusu Kuku wa Kisasa(Chotara)...1️⃣Kuku Chotara Ni Kuku Wanaofanya Vizuri Katika Soko...
08/01/2026

JE WAJUA...???
🐓🐓
🗣️Ukweli Usioujua Kuhusu Kuku wa Kisasa(Chotara)...

1️⃣Kuku Chotara Ni Kuku Wanaofanya Vizuri Katika Soko Kwa Upande Wa Nyama Na Mayai...

2️⃣Ni Kuku Ambao Wanachukua Mda Mfupi Na Kuwa Tayari Kuingia Sokoni Yaani Ndani Ya Miezi 2½ Hadi 3 Wanakua Tayari Kwa Kitoweo...

3️⃣Ni Kuku Ambao Wanataga Mayai Mengi Kwa Mwaka Yaani Wanauwezo Wa Kutaga Mayai 100 Hadi 250 Kwa Mwaka...

4️⃣Mayai Yake Yanafaa Kutotolesha Endapo Umewachanganya Majike Na Majogoo Na Ukapata Vifaranga Vizuri Tu...

5️⃣Kuku Chotara Anauwezo Wa Kujitafutia Chakula K**a Kuku Wa Kienyeji Kwahiyo Anaweza Kuishi K**a Kuku Wa Kienyeji...

6️⃣Kuku Chotara Anakua Na Uzito Mkubwa Kuliko Aina Yoyote Ya Kuku Wanauwezo Wa Kufikisha 4Kg Hadi 8Kg Endapo Utawafuga Vizuri Na Kuwapa Chakula Kizuri...

7️⃣Kuku Chotara Ananyama Tamu Akitoka Kuku Wa Kienyeji Anafata Kuku Chotara Kwa Nyama Yenye Radha Nzuri Zaidi...

8️⃣Kuku Chotara Hawezi Kuatamia Mayai Yake Yeye Anataga Tu Kwahiyo Ukiona Kuku Wako Anataga Tu Bila Kuatamia Ujue Ni Chotara...

9️⃣Kuku Chotara Amekua Na Faida Kubwa Kwa Wafugaji Kwasababu Ya Uwezo Wao Mkubwa Wa Kutaga Mayai Mengi Na Kukua Kwa Haraka Kwahiyo Imefanya Wawe Na Mzunguko Wa Haraka Wa Pesa...

🔟Mwisho Kabisa Wanauwezo Mkubwa Wa Kustahimili Magonjwa Akitoka Kuku Wa Kienyeji Anafata Kuku Chotara Kwa Uwezo Wa Kustahimili Magonjwa...

🙏 Hongera Sana Naamini Sasa Umeshajua

Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774

🚫...KINACHOKUKWAMISHA KUFANIKIWA KATIKA SAFARI YAKO YA UFUGAJI NI TAMAA ILIYOPITILIZA...🙆💁Kikawaida Binadamu Tumeumbwa N...
08/01/2026

🚫...KINACHOKUKWAMISHA KUFANIKIWA KATIKA SAFARI YAKO YA UFUGAJI NI TAMAA ILIYOPITILIZA...🙆

💁Kikawaida Binadamu Tumeumbwa Na PUPA AU TAMAA AU KUPENDA MAFANIKIO YA HARAKA...

🙂‍↕️...Hali Hii Imechangia Kwa Kiasi Kikubwa Sana Wewe 🫵 KUTOFANIKIWA KATIKA SAFARI YAKO YA UFUGAJI...

🐓...Ebu Jiulize Swali Kisha Majibu Yabakie Katika Akili Yako...👇

"""KWANINI UKIANZA UFUGAJI KWA KUKU WACHACHE UNAOWEZA KUWAHUDUMIA VIZURI NA KUWAPA MATUNZO YA UHAKIKA UNAKUA NA ASILIMIA KUBWA ZA KUFANIKIWA ILA TU... PALE UNAPOANZA KUINGIZA TAMAA YA KUPATA ZAIDI YA UWEZO WAKO UNAANGUKIA PUA👃...???"""

💔 Wafugaji Wengi Sana UKIWEMO NA WEWE NDANI YAKE Mnapotaka Kuanza Ufugaji Wa Kibiashara Mnakua Na Matamanio Makubwa Sana Yanayoambatana Na Speed(Kasi) Kubwa Sana Ambayo Siku Ya Siku Unajikuta UNAKOSA YOTE Yaani Wahenga Wanasema Hivi...👉"TAMAA MBELE MAUTI NYUMA" Yaani Ukitanguliza Kufanya Ufugaji Kwa Tamaa Basi ANGUKO KUBWA LIPO NYUMA YAKO...

✍️...Aya Twende Taratibu Ili Tuelewane Chukua Hii Kauli Kisha Ishi Nayo...👇

🧑‍🏫JIWAZIE MAKUBWA KATIKA MAFANIKIO YAKO YA UFUGAJI ILA NENDA POLEPOLE KWA KUFATA MCHAKATO UNAVYOHITAJI...

🗣️ TUNARUDI TENA KWA SAUTI NDOGO ILI UTUELEWE NI HIVI...👇
..Jiwazie Makubwa Katika Safari Yako Ya Ufugaji Ila Nenda Polepole Kwa Kufata Mchakato Unavyohitaji...

🌠Maana Yetu Ni Kwamba Unapotaka Kuanza Ufugaji Wa Kibiashara Hakikisha Unajifanyia Tathimini Ya Uwezo Ulionao Kwasasa Kisha Anza Kulingana Na Uwezo Halisi Na Sio Kulazimisha Vitu Ambavyo Vipo Nje Ya Uwezo Wako...

🐣Hatukatai Kwamba Ukifuga Kuku Wengi Na Faida Inakua Kubwa Pia Ila Je...???

🤷Kwasasa Unaelimu Ya Kutosha Ya Kufuga Idadi Kubwa Ya Kuku...???

🤷Unauhakika Wa Kusimamia Mradi Wako Kwa Hatua Hiyo Unayoitaka...???

🤷Unafahamu Namna Ya Kufuga Kuku Kwa Ufasaha Ili Kufikia Malengo Unayohitaji...???

🤷Au Unaamini Pesa Ndio Kila Kitu Kwahiyo Atak**a Hauwezi Ila Kwasababu Pesa Unayo Utaweza Tu...???

🤷Ushawahi Kufuga Japo Kwa Uchache Ili Kutambua Namna Ya Ufugaji Unavyoenda Au Ndio Unaenda Kufuga Kwa Zile Kauli Za High Risk High Profit Yaani Ukithubutu Kwa Ukubwa Zaidi Na Faida Utapata Kubwa Zaidi...

🤷Shida Yako Ni Kufanikiwa Mara Moja Au Unataka Kufanikiwa Kwa Muda Mrefu Katika Hii Safari Yako Ya Ufugaji...???

MASWALI Ni Mengi Hatuwezi Uliza Yote Ila Hapo Unachotakiwa Wewe Kukibeba Ni Kukubali Kuanza Ufugaji Kwa Malengo Na Sio Mihemko Ya TAMAA ILIYOPITILIZA...

💁Andaa Plan Yako Ya Ufugaji Kisha Jilizishe Iko Sawa Yaani Mpango Wako Haujaambatana Na TAMAA ZA MUDA MFUPI Zinazoweza Kukukwamisha Baada Ya Hapo Washirikishe Watu Unaowaamini Kisha Anza...

💓💔💓HAKUNA KITU KIZURI DUNIANI KINACHOLETA MAFANIKIO YA UHAKIKA K**A KUFANYA VITU VYAKO KWA UTULIVU WA NAFSI YAANI UNAPANGA MIPANGO YAKO TARATIBU KWA KUTARAJIA MATOKEA MAKUBWA SIKU ZA USONI...

😭🥳😭HAKUNA KITU KIBAYA KINACHOKATISHA MALENGO YA WAFUGAJI WENGI K**A TAMAA YAANI KUPANGA MIPANGO YAKO BILA UTULIVU WA NAFSI WEWE UNAUSIKILIZA MOYO UNAVYOTAKA MATOKEO KWA PUPA NA HATIMAE UNATENGENEZA VIKWAZO VYA KUKUFANYA USIFIKIE NDOTO ZAKO KWA TAMAA ZA MUDA MFUPI TU...

🫂 Tunakupenda Sana Tena Zaidi Ya Sana Ombi Letu Kwako Tuliza Akili Yako Kuna Mafanikio Makubwa Yapo Mbele Yako Ukiamua Kuwa Mtulivu Wa Mipango Yako Ikaendana Na Uhalisia...

🌳🌲ATA MBUYU ULIANZA K**A MCHICHA JIPE MUDA UTAFIKA TU HUKO UNAPOTARAJIA KUFIKA INSHALLAH...🙏

Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774

Kuvimba macho kwa kuku ni dalili ya ugonjwa, si ugonjwa pekee.Hii hali huletwa na vitu kadhaa, mara nyingi ikiambatana n...
08/01/2026

Kuvimba macho kwa kuku ni dalili ya ugonjwa, si ugonjwa pekee.
Hii hali huletwa na vitu kadhaa, mara nyingi ikiambatana na mafua, kukohoa, au kutokwa na k**asi puani.

🐔 Sababu Kuu za Kuku Kuvimba Macho

1. Coryza (Infectious Coryza)

Huu ndio ugonjwa maarufu zaidi unaosababisha macho kuvimba.

Dalili:

Macho kuvimba upande mmoja au wote.

Kutoka k**asi puani, harufu mbaya puani.

Kuku hawataki kula, wanakuwa wazito, wanakohoa.

Husababishwa na bakteria (Haemophilus gallinarum).

2. Chronic Respiratory Disease (CRD / Mycoplasma)

Dalili:

Kuvimba macho, kupumua kwa shida.

Kukohoa, kutoa sauti ya “gurgle” wanapopumua.

Kukosa hamu ya kula.

Husababishwa na Mycoplasma gallisepticum.

3. Mazingira Mabaya

Banda lenye vumbi, baridi, moshi, au upepo mkali pia linaweza kusababisha macho kuvimba (hasa bila maambukizi).

4. Vimelea au vumbi kuingia machoni

Kuku wakipiga manyoya au kuchakura kwenye udongo wenye vumbi, macho yanaweza kuvimba kwa muda mfupi bila ugonjwa.

💊 Matibabu Unayoweza Kufanya

1. Tumia antibiotic

Dawa nzuri ambazo hupatikana kirahisi madukani ni:

Tylodox

Doxycycline + Tylosin

Erythromycin

Oxytetracycline (Oxyvit, Alamycin, Terramycin)

Tumia kwa siku 5–7 kwenye maji ya kunywa.

2. Weka multivitamin

Weka Vitalyte, Aminovit, au Super-Vit kusaidia kuku kupata nguvu na kuongeza kinga.

3. Tibu macho moja kwa moja

Osha macho kwa maji safi vuguvugu + chumvi kidogo (saline solution).

Kisha paka ointment ya macho ya antibiotic k**a Terramycin eye ointment.

4. Weka mazingira safi

Banda liwe kavu, lenye hewa ya kutosha (bila upepo wa moja kwa moja).

Safisha mara kwa mara ili kupunguza bakteria.

⚠️ Kuzuia Kuambukiza

Ugonjwa huu huambukiza haraka sana.
➡️ Watenganishe kuku wagonjwa na wazima.
➡️ Safisha vyombo vya chakula na maji kila siku.
➡️ Rudia chanjo ya Lasota baada ya kupona kwa kuku waliobaki wazima.

Karbu ufuge na Tumwesige Mixed Farm +255714887774

Address

+255714887774
Dodoma

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tumwesige Mixed Farm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category