03/12/2025
BIASHARA YA MADINI....
Imeandikwa Madini Yetu Tanzania Limited
Kisheria hapa Tanzania 🇹🇿 ili mtu aweze kufanya biashara ya kununua madini na kuuza madini ni lazima awe na leseni,
bila kuwa na leseni k**a mtu atanunua madini na kuuza madini basi mtu huyo anavunja sheria na mtu huyo akibainika atak**atwa na kushtakiwa katika vyombo vya sheria.., na huko anaweza pewa adhabu ya kulipia faini na kifungo
Ili mtu aweze kufanya biashara ya kununua madini na kuuza lazima awe na moja kati ya leseni mbili zifuatazo:
01: leseni ya broker (leseni ndogo)
02: leseni ya dealer (leseni kubwa)
HEBU IFAHAMU HII LESENI NDOGO YA BROKER...
Hii leseni inaitwa leseni ndogo kwa kuwa hii leseni ni maalumu kwa ajili ya watanzania tuu ambao wana mitaji mdogo midogo , leseni hii haitolewi kwa wageni toka nje ya nchi kidupi leseni hii hapewi mtu k**a sio raia wa Tanzania 🇹🇿
Leseni hii ukiwa nayo:
>> madini utanunua Tanzania na kuyauza hapahapa Tanzania, leseni hii hairuhusu wewe kutoka madini nje ya mipaka ya Tanzania 🇹🇿
>> leseni unatakiwa kuikata katika ofisi za madini za mkoa unaotaka ukannunulie madini yako na leseni hii itatumika kununulia madini katika mkoa huo tuu, kma unataka ukanunue madini geita basi nenda ofisi za madini za geita kakate leseni hii, na leseni hii utaitumia kununua madini mkoa wa geita tuu, ukitaka kununua madini shinyanga leseni ya geita haitambuliki nenda tena shinyanga kakate leseni ingine na huko..,
>> leseni hii inadumu kwa mwaka 1 tuu, na mnatakiwa muanze kukata leseni hii kila unapoingia mwaka mpya wa fedha yani July 1 kwa maana kila mwaka wa fedha unapoisha na leseni zote zinaisha na mtatakiwa ku renew upya leseni zenu k**a utahitaji kuendelea na bishara.., ukikata leseni February ujue ikifika July 1 leseni hiyo imeisha muda wake,
>> utanunua madini katika mkoa uliokatia leseni, ila katika kuuza unaweza enda kuuza katika soko la mkoa wowote utakalo ila sharti muhimu kabla hujasafirisha madini yako katika mkoa ulioyanunulia sheria inaku