13/05/2026
JINSI YA KUTOKA KUWA MFUGAJI WA KUDHARAULIWA HADI MFUGAJI WA KUHESHIMIWA KIBIASHARA
Wazee wetu walisema, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Lakini kwenye ulimwengu wa biashara, ukifanya mambo kinyonge utadharaulika tu. Mfugaji anayedharauliwa ni yule anayefuga kuku wachafu, banda linanuka mtaa mzima, kuku wanakufa kila siku, na mwisho wa siku hana faida yoyote mfukoni. Anaitwa mfuga kuku kwa sababu hana kingine cha kufanya.
Leo nataka nikupe siri ya namna ya kubadili upepo na kuwa mfugaji wa kibiashara anayeheshimika, ambaye watu wanatamani kujua siri ya mafanikio yake.
1. ACHA KUFUGA KWA MAZOEA, ANZA BIASHARA
Mfugaji anayedharauliwa huwa hana hesabu. Hajui kuku wamekula kiasi gani na wameingiza kiasi gani. Mfugaji wa kuheshimiwa anajua kuwa kila punje ya chakula ni uwekezaji. Ili uheshimike kibiashara, lazima uwe na takwimu. Unapoongea na mteja au benki, unawaambia namba: Nina kuku 50, kila mmoja ana uzito wa kilo 3, na gharama yangu ya uzalishaji ni ndogo kwa sababu ninatumia Azolla na funza. Hapo heshima inaanza.
2. MIFUMO YA KISASA (CAGES) NDIO SURA YA BIASHARA
Ukifuga kuku chini kwenye sakafu chafu, utaonekana mchafu. Lakini ukiweka mfumo wa cage (mabanda ya kisasa), biashara yako inapata sura mpya. Kuku wanakuwa wasafi, mayai yanatokea yakiwa masafi, na magonjwa yanapungua kwa asilimia 90. Wageni wakija kuona mradi wako, hawazibi pua. Wanaona uwekezaji makini. Hapo ndipo unapotoka kwenye kuitwa mfuga kuku na kuanza kuitwa mkurugenzi wa mradi.
3. SAA YA KAZI NA UDAKU NI TOFAUTI
Mfugaji wa kibiashara anayeheshimika ana nidhamu ya muda. Haitaji kukaa bandani kutwa nzima. Kwa kutumia mifumo ya automatiki, unatumia dakika 20 tu kwa siku kuhudumia kuku 50 au 100. Muda uliobaki unautumia kutafuta masoko na kupanua biashara. Watu wakikuona unafanya kazi kidogo lakini unapata matokeo makubwa, lazima wakuheshimu na kukuita mwerevu.
4. MKAMIA MAJI HAYANYWI: PUNGUZA GHARAMA ILI UPATE FAIDA
Heshima kubwa ya mfanyabiashara ipo kwenye faida anayopata. Ukitegemea chakula cha dukani pekee ambacho bei yake inapanda kila siku, utabaki unalalamika na watu watakucheka. Mfugaji wa kuheshimiwa anazalisha chakula chake mwenyewe kwa kutumia Azolla na funza. Badala ya kutumia 192,000/- kwa mwezi, unatumia 50,000/- tu. Ile laki moja na nusu unayookoa ndiyo inayonunua gari, inajenga nyumba, na kupeleka watoto shule nzuri. Hapo heshima inakuja yenyewe bila kuombwa.
5. KUWA MTAALAMU WA KILE UNACHOFANYA
Mtu anayejua anachokifanya huheshimiwa siku zote. Usikubali kuwa mfugaji ambaye hajui hata chanjo ya kideri inatolewa lini. Jiunge na madarasa ya kitaalamu ili uongeze maarifa. Jifunze sayansi ya kuku kukua haraka na kufikisha kilo 3 ndani ya muda mfupi. Unapokuwa na majibu ya changamoto za bandani kwako, unakuwa kioo cha jamii.
Ufugaji wa kibiashara sio miujiza, ni maarifa na mifumo. Ukiamua kuachana na ufugaji wa mazoea na kufuata ramani yetu ya banda la kuku 50, utabadili maisha yako ndani ya muda mfupi sana.
Je, upo tayari kuacha kudharauliwa na kuanza kuheshimika k**a mfanyabiashara mkubwa wa kuku?
Wasiliana NASI LEO
0693 410 074 (Jomo Kuku farm)
0670 340 708 (Jomo Poultry Farm)