18/05/2024
*1.* Kunyamaza wakati fulani maishani mwako siyo kipawa bali ni nidhamu
*(1 Wathesalonike 4: 11).*
*2.* Nyamaza unapohisi hasira
*(Mithali 14:17).*
*3.* Nyamaza unapokuwa huna taarifa ya kutosha au ukweli kuhusu unachotaka kusema *(Mithali 18:13).*
*4.* Nyamaza unapokuwa ni wakati wako kusikiliza na kujifunza
*(Mithali 13: 1).*
*5.* Nyamaza ukigundua kwamba maneno yako yataleta picha mbaya
*(Mithali 17: 27).*
*6.* Nyamaza ukijua kile unachotaka kusema kitaharibu jina na sifa ya mwenzio
*(Mithali 16: 27).*
*7.* Nyamaza ukijua utakachosema kitaharibu urafiki na kujeruhi mwenzako
*(1Wakorintho 15: 33).*
*8.* Nyamaza ukigundua kwamba utaaibika baadaye kwa sababu ya ulichokisema
*(Mithali 8:8).*
*9.* Nyamaza ukijua unachotaka kusema kitamdhalilisha Mungu, wewe mwenyewe au familia yako
*(1Petro 2: 21-23).*
*10.* Nyamaza ikiwa wakati ulio nao ni wakati wa kazi
*(Mithali 14: 23).*
*11.* Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, atajilinda nafsi yake na taabu
*(Mithali 21: 23).*
Mungu akupe neema ya kujenga nidhamu ya kunyamaza kwa maana maneno ya kinywa chako ni mtego kwako
*(Mithali 6:2).*
#๐ช๐ฏ๐จ๐ต๐ฎ๐ฌ๐๐ถ๐ผ๐น๐ด๐ฐ๐ต๐ซ๐บ๐ฌ๐ป๐ญ๐ถ๐น๐บ๐ผ๐ช๐ช๐ฌ๐บ
#๐จ๐ต๐ฎ๐จ๐ณ๐ฐ๐จ๐ฒ๐ฌ๐บ๐ฏ๐ถ๐๐จ๐ฒ๐ถ
#๐ป๐ฐ๐ด๐ฌ๐ป๐ถ๐ช๐ฏ๐จ๐ต๐ฎ๐ฌ
#๐๐๐
๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐
#๐ฏ๐ฐ๐ฝ๐๐ถ๐ป๐ผ๐๐จ๐จ๐ต๐ฐ