11/05/2026
Farm For the Future tumetembelewa Mheshimiwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo (DED), ambaye alipata wasaha wa kutembelea shamba na kuvutiwa sana na maendeleo ya kilimo cha kisasa cha kibiashara pamoja na programu za kijamii zinazotekelezwa na FFF, ikiwemo Children Farm na Goat Milk for Profit and Nutrition.
Mkurungenzi alionesha kuridhishwa na ubunifu, mazingira ya kujifunzia kwa vitendo, pamoja na mchango wa FFF katika maendeleo ya jamii kupitia miradi yake mbalimbali. Katika mazungumzo hayo, alisisitiza umuhimu wa kuanzisha utalii wa kilimo (Agro-tourism) ili watu mbalimbali waweze kutembelea shamba, kujifunza mbinu za kisasa za kilimo na kupata uzoefu wa moja kwa moja.
K**a hatua kubwa ya maendeleo, DED ameahidi kutoa ushirikiano wa karibu kuhakikisha taratibu zote za kiserikali zinazohitajika zinakamilika ili wanafunzi waendelee kutembelea Children Farm na kupata elimu ya kilimo kwa vitendo.
Ziara hiyo ni mafanikio makubwa kwa FFF katika kuendelea kujenga ushirikiano, kuhamasisha ubunifu wa kilimo, na kuleta matokeo chanya yenye manufaa kwa jamii.