17/02/2024
Swali ambalo watu wengi wamekua wakiamini ni kuwa ili Tetea atage mayai lazima awepo Jogoo wa Kumpanda ndio Yai lipatikane. K**a wewe ni miongoni mwa watu wanaoamini hivyo basi hili Somo ni kwaajili yako kwa sababu unachokiamini sio sawa.
Tetea akifikisha weeks 16-18 anakua tayari ameshaanza kuonyesha dalili za kuanza kutaga kwa ktoa mlio wa kutetea (Ishara ya kuku kupevuka kwaajili ya kuanza kutaga)
Mfumo wa utagaji moja kwa moja (Automatically) uanza mchakato wa kutengeneza yai na inachukua masaa 24-26 yai kujitengeneza lenyewe.
Yai likishakua tayari tetea anataga baada ya hapo inachukua Dakika 30 mfumo kuanza kutengeneza yai liingine.
Kwahiyo tetea yoyote awe wa kisasa au wa kenyeji mda wa kutaga ukifika haiitaji Jogoo ili atage ni kiitendo cha Asili Yai Kujitengeneza Lenyewe...
*SASA SWALI LINAKUJA JE JOGOO ANAKAZI GANI K**A TETEA ANAWEZA KUTAGA MWENYEWE BILA KUPANDWA NA JOGOO??
Jibu ni kwamba Jogoo ndiye mwenye uwezo wa kurutubisha yai na kulifanya liwe na uwezo wa kutoa kifaranga.
MUHIMU:
TETEA HUTAGA YAI MOJA KWA SIKU,NA PIA ANARUKA MARA MOJA KWA WIKI HATAGI YAI