The Kingdom of Heaven

The Kingdom of Heaven MISSION - Preaching and teaching the good news of the Kingdom of Heaven.

08/18/2026

URAIA WETU SIO WA DUNIANI KATIKA NCHI YEYOTE ILE, BALI URAIA WETU NI WA MBINGUNI KATIKA KRISTO.

“Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo; atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake” (Waefeso 3:20-21).

Ndugu zetu, sisi tuliozaliwa mara ya pili na Roho Mtakatifu wa Mungu, uraia wetu ni wa Mbinguni na sio duniani.

K**a vile;

👉🏽 Watanzania ni raia wa Tanzania
👉🏽 Wakenya ni raia wa Kenya
👉🏽 Waganda ni raia wa Uganda
👉🏽 Wamarekani ni raia wa Marekani

Vivyo hivyo pia na;

👉🏽 Wakristo ni raia wa mbinguni ndani ya Kristo

Biblia inasema, sisi tuko ndani ya Kristo, na ndani ya Kristo tunaishi, tunakwenda, na kuwa na uhai wetu (Matendo 17:28). Maana yake Kristo ni nchi na ni makao ya watu wa Mungu katika ulimwengu wa Roho, k**a vile nchi zingine zilivyo katika dunia hii.

Hivyo sisi kuitwa wa-kristo maana yake sisi ni raia wa nchi inayoitwa Kristo. Na nchi hii inayoitwa Kristo ndio nchi ya mbinguni. Kuwa ndani ya Kristo ndio kuwa ndani ya nchi ya mbinguni.

Lakini Kristo sio tu ni nchi yetu mpya, bali pia ndio mwili wetu mpya wa Roho. Kuwa ndani ya Kristo, ni kuwa ndani ya mwili mpya wa Roho wa mbinguni. Kuwa katika Kristo, maana yake tumevua sasa mwili wa nyama (wa duniani) na tumevaa mwili mpya wa Roho (wa mbinguni).

“Katika yeye mmetahiriwa kwa tohara isiyofanyika kwa mikono, kwa kuuvua mwili wa nyama, kwa tohara ya Kristo” (Wakolosai 2:11).

Tulipoletwa duniani Mungu alitupatia mwili wa duniani (mwili ya nyama), na alipokuja kutuokoa na kututoa duniani akatupatia mwili mpya wa mbinguni (mwili ya Roho).

“Hupandwa mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko. Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha.

Lakini hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili; baadaye huja ule wa roho. Mtu wa kwanza atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni.

K**a alivyo yeye wa udongo, ndivyo walivyo walio wa udongo; na k**a alivyo yeye wa mbinguni, ndivyo walivyo walio wa mbinguni. Na k**a tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni.

Ndugu zangu, nisemayo ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika” (1 Wakoritho 15:44-50).

Anasema hapo juu;

“Mtu wa kwanza atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni.

K**a alivyo yeye wa udongo, ndivyo walivyo walio wa udongo; na k**a alivyo yeye wa mbinguni, ndivyo walivyo walio wa mbinguni,”

maana yake, k**a “Mtu wa pili atoka mbinguni” ndivyo hivyo pia na sisi “walio wa mbinguni” tumetokea mbinguni.

07/22/2026

MAKUHANI WA KIFALME WANAHUDUMU KATIKA HEKALU LA MUNGU LA MBINGUNI NA SIO DUNIANI

“…..ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi” (Ufunuo 5:9b-10).

“Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme…..” (1 Petro 2:9).

Maneno hayo ☝️yanasema Yesu alitununua sisi kwa damu yake na kutufanya kuwa MAKUHANI WA KIFALME kwa Mungu.

Sisi k**a Makuhani wa Kifalme wa Agano Jipya la KIROHO au la ROHONI, tunahudumu katika hekalu la ROHONI la Mbinguni na sio katika hekalu la MWILINI la duniani.

Yesu k**a Kuhani wetu Mkuu, anahudumu katika hekalu la Mbinguni na sio la duniani.

Neno linasema;

“Tunaye kuhani mkuu wa namna hii, aliyeketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Ukuu mbinguni, mhudumu wa patakatifu, na wa ile hema ya kweli, ambayo Bwana aliiweka wala si mwanadamu” (Waebrania 8:1-2).

Katika hekalu hilo Kuhani wetu Mkuu anapohudu, ndipo na sisi makuhani tulio chini yake tunahudumu pamoja naye hapo.

Kumbuka Yeye na sisi tumeungana na kuwa Roho moja naye. Kumbuka Yeye ni kichwa na sisi ni mwili wake, Kichwa + Mwili = Mtu mmoja aliye kamili. Kumbuka pia sisi tuko ndani yake, hivyo alipo Yeye ndipo tulipo na sisi, anapohudumu Yeye ndipo na sisi hapo hapo tunapohudumu pamoja naye.

Hivyo k**a Yeye “ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Ukuu mbinguni”, ndivyo na sisi tumeketi pamoja naye hapo. Na k**a Yeye ni “mhudumu wa patakatifu, na wa ile hema ya kweli, ambayo Bwana aliiweka wala si mwanadamu,” na sisi pia tu wahudumu pamoja naye katika hema hiyo hiyo.

Hapo ndipo sisi k**a makuhani wa kifalme tunapotakiwa kuwepo kiroho na kutoa huduma hapo za kiroho mbele za Mungu kwanza, na kutokea hapo kwenda kwa watu ulimwenguni kote. Mungu awabariki sana. Amina!!

07/20/2026

KUKAA NA KUISHI NA MUNGU KATIKA MAKAZI YAKE YA MBINGUNI SASA TUKIWA DUNIANI

“BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. BWANA Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya” (Mwanzo 2:7-8).

Mungu alipomuumba mwanadamu alimweka katika Bustani ya Edeni, hakumweka mahali pengine popote pale. Bustani ya Edeni katika sehemu zingine katika maandiko, inaitwa bustani ya Mungu (Ezekieli 28:13;31:8-9), inaitwa Sayuni (Isaya 51:3), inaitwa mlima Mtakatifu wa Mungu (Ezekieli 28:14,16).

Inaitwa pia “Paradiso” (Ufunuo 2:7) na “Yerusalemu mpya” (Ufunuo 22:2) kwa sababu ya mti wa uzima uliokuwa ndani yake. Inaitwa pia Mbinguni Yerusalemu mpya iko mbinguni. Kwa hivyo Mungu alipomuumba mwanadamu alimweka katika bustani yake, katika mlima wake Mtakatifu, katika Paradiso, ndani ya mbinguni, ili tuishi huko tukiwa duniani.

Mungu alimweka mwanadamu katika bustani yake, katika makao yake mwenyewe ili aweze kuishi naye mahali Yeye anapoishi mbinguni akiwa duniani. Hilo ndilo Mungu alilolikusudia tangu mwanzo, kuishi pamoja na watu wake mahali anapoishi Yeye tukiwa duniani. Mungu hakukusudia watu waishi nje ya Yeye alipokuwa anaishi. Ndio maana mtu kabla ya kutenda dhambi, Mungu hakukusudia kumtoa mtu katika bustani yake hiyo.

Mtu alipotenda dhambi, ndipo Mungu alipomtoa katika bustanini yake, katika makao yake, katika Paradiso yake - mbinguni kwake, na kuanza kuishi duniani tu bila ya kuwa mbinguni. Yesu alipokuja kulipa gharama ya dhambi za watu waliofanya, na kutufanya tena wenye haki, kusudi lake ni kuturudisha sisi tena katika bustanini yake, katika makao yake tena, mbinguni kwake tena ili tuweze kuishi pamoja naye tena huko tukiwa duniani.

Hilo ndilo Yesu alilofanya na kulikamilisha katika ulimwengu wa Roho, alipokufa na kufufuka na kuketishwa mbinguni kwa ajili yetu (Waefeso 2:4-6). Tayari tumesharudishwa kwa Mungu sasa katika bustani yake, katika makao yake - Mbinguni, ili tuishi kutokea mbinguni duniani. Tayari tumesharejeshwa mbele zake mahali Yeye alipo. Tumesharejeshwa katika uwepo wake. Yeye alipo sasa ndipo na sisi pia tulipo sasa. Hili tayari limeshafanyika katika Kristo, si kana kwamba tunasubiri lifanyike katika siku zijazo.

K**a hili tayari limeshakuwa katika Kristo, basi tunahitaji kuamini na kuanza kuishi humo sasa pamoja na Yeye katika Roho, huku tukiwa duniani. Tayari tumesharudishwa mbinguni sasa katika bustani yake, na tunaishi pamoja naye sasa katika bustani yake k**a alivyokusudia tangu mwanzo.

Si kwamba tuko njiani tunakwenda huko sasa, bali tayari tumeshafika sasa katika mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni. Neno linasema, “Bali ninyi mmeshafika katika mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi, mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika, na Yesu mjumbe wa agano jipya….” (Waebrania 12:22-24).

Hapo ndipo Mungu anasema, hayo ndio makazi yetu sisi na Yeye. Neno linasema, “Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, k**a bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe. Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao” (Ufunuo 21:2:3).

07/09/2026

MUNGU ALIKUSUDIA WANA WAKE KUWA NDIO WATAWALA WA ULIMWENGU

“Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa sura yetu, kwa mfano wetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi” (Mwanzo 1:26).

Katika mstari wetu wa ufunguzi, watu waliye na sura na mfano wa Mungu ni wana wake. Na wana wake ndio hao Mungu amesema hapo alikusudia wawe watawala wa ulimwengu, na sio watu wasio wana wake.

Utawala huu Mungu aliowapatia wana wake katika ufalme wake wa rohoni, ulikuwa ni wa ulimwengu wa rohoni kwanza na pia katika ulimwengu wa mwilini. Hii ndio maana unaona Yesu alisema, “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani” (Mathayo 28:18), kwa ajili yetu sisi.

Na hiyo ndio mamlaka ya jina la Yesu aliyopewa kwa ajili yetu. Neno linasema, “Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba” (Wafilipi 2:9-11).

Hiyo ☝️ndio mamlaka yetu, Yesu aliyopewa kwa ajili yetu wana wa Mungu, na akatupatia sisi mamlaka hiyo ili tuweze kutawala vitu vyote vya mbinguni, duniani, na chini ya nchi. Hiyo ndio mamlaka tunayotakiwa kuitumia kutawala vitu vyote vya mbinguni, duniani, na chini ya nchi, ili kusimamia mapenzi yake yaweze kutimia katika maeneo yote hayo. Mungu awabariki sana nyote. Amina!!

07/06/2026

NJIA PEKEE YA KUTUMIA KUIKOMBOA TANZANIA NI NJIA YA MUNGU NA SIO YA DUNIA

“Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo” (Matendo 4:12).

Ndugu zangu, njia pekee na ya kweli ya kuikomboa Tanzania ni njia ya Mungu na sio ya dunia. Katika mstari wetu wa ufunguzi, Neno la Mungu linasema, “hakuna wokovu (ukombozi) katika mwingine awaye yote, zaidi ya katika Yesu tu.” Anasema, “kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”

Hivyo kutafuta kuiokomboa Tanzania bila ya kumtumia Yesu, na uwezo wake, na kutumia njia zake, hatuwezi kuikomboa Tanzania kutoka kwa adui. Yesu ndiye pekee tuliyepewa na Baba kuja kutukomboa kutoka kwa adui Shetani. K**a vile kila mtu bila Yesu hakuna wokovu, ndivyo hivyo pia kila Taifa ua nchi bila Yesu hakuna wokovu.

“Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu” (1 Yohana 4:14).

Na Yesu alipokuja kuuokoa ulimwengu kutoka kwa adui, hakutumia njia za duniani za kivita za kimwili, bali alitumia njia za Mungu za kiroho. Maana adui Shetani ni wa rohoni na sio wa mwilini. Vivyo hivyo na Tanzania pia, adui wa kweli wa Tanzania ni wa rohoni na sio wa mwilini. Hivyo kuikomboa Tanzania tunapaswa kutumika njia za Roho wa Mungu za rohoni na sio njia za roho ya Shetani za mwilini.

Neno linasema, “Kwa maana vita vyetu sisi si juu ya damu na nyama (wanadamu); bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho” (Waefeso 6:12).

“Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia” (Mathayo 12:28).

K**a Mungu anatuambia, vita vyetu sio dhidi ya wanadamu bali dhidi ya roho za giza, hivyo vita yetu sio ya kimwili bali ni ya kiroho. Wanadamu wanatumiwa tu na roho za giza kutenda mabaya kwa wengine, hivyo hao sio maadui zetu bali ni roho hizo za giza zinazowatumikisha hao watu kufanya hayo mabaya. Hii ndio sababu Yesu alisema, “Baba wasamehe hao” watu walionisubisha “maana hawajui walitendalo.” Halafu akaenda akamshughulikia Shetani kuzimu na kumshinda na kutoka kuzimu akiwa amepata ushindi wa wokovu.

Hivyo tusiwachukie wanadamu hata hao tunaoona k**a maadui zetu. Hii ndio sababu kwa nini Yesu alisema, “Lakini nawaambia ninyi…..Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi, wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi” (Luka 6:27-28).

“Maana mkiwapenda wale wawapendao ninyi, mwaonyesha fadhili gani? Kwa kuwa hata wenye dhambi huwapenda wale wawapendao. Nanyi mkiwatendea mema wale wawatendeao mema, mwaonyesha fadhili gani? Hata wenye dhambi hufanya vivyo hivyo. Na mkiwakopesha watu huku mkitumaini kupata kitu kwao, mwaonyesha fadhili gani? Hata wenye dhambi huwakopesha wenye dhambi, ili warudishiwe vile vile.

Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo, na thawabu yenu itakuwa nyingi; nanyi mtakuwa wana wa Aliye juu, kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasiomshukuru, na waovu. Basi, iweni na huruma, k**a Baba yenu alivyo na huruma” (Luka 6:32-36).

Hivyo tusifanye vita na wanadamu kwa sababu hao sio maadui wetu, bali tufanye vita na Shetani pamoja na roho zake za giza katika ulimwengu wa rohoni na kumshinda na kupata ushindi wa kuikomboa nchi na Taifa.

Na Maombi ni mojawapo ya silaha kubwa sana tunayotakiwa kutumia kupigana vita na Shetani. Tuombe sana ndugu zetu Ili kumshughulikia adui kwa umoja na kumshinda. Mungu awabariki sana. Amina!!

07/05/2026

YESU ANASEMA: HUWEZI KUMTOA SHETANI KWA KUMTUMIA SHETANI

Yesu; “aliletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona” (Mathayo 12:22).

“Lakini Mafarisayo waliposikia [Yesu amemponya mtu mwenye pepo], walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo” (Mathayo 12:24).

Yesu akawaambia;

“Awezaje Shetani kumtoa Shetani?” (Marko 3:23).

Maana yake huwezi kumtoa pepo (Shetani) kwa kumtumia mkuu wa pepo (Shetani).

Yesu akawaambia pia ni kwa nini hatuwezi kumtoa Shetani kwa kumtumia Shetani. Akasema;

“Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama. Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje?” (Mathayo 12:25-26).

Halafu akawaambia;

“Mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo hao ndio watakaowahukumu” (Mathayo 12:27).

Yesu alisema hilo kutuonyesha kuwa, wana wa Shetani ndio hutoa pepo kwa mkuu wa pepo, lakini Yeye hatoi pepo kwa mkuu wa pepo.

Halafu akawapa jibu, akawaambia;

“Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia” (Mathayo 12:28).

Yesu hapo aliwaambia namna Yeye anayotoa pepo (Shetani) - akasema kwa Roho wa Mungu. Na akasema Yeye anapotoa Shetani kwa Roho Mungu, ndio mjue ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia au umeshakuja ili kuwapatia haki yenu mliyoibiwa, mliyokuwa mnaitafuta.

Na mwisho Yesu akasema;

“Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake” (Mathayo 12:29).

Maana yake hutuwezi kwenda kwa Shetani mwenye nguvu, pasipo kuwa na nguvu kubwa zaidi ya Roho wa Mungu kuliko yake na kumfunga kwanza Shetani, na ndipo tutaweza kuteka nyumba yake.

Hatuwezi kumtoa Shetani mwenye nguvu juu ya Tanzania k**a hatutatumia nguvu za Roho wa Mungu kumfunga na kuichukua Tanzania toka kwake.

Yesu ametuonyesha hapo kuwa, hakuna nguvu ya ki-binadamu inayoweza kumshinda Shetani. Yesu mwenyewe amesema hakutumia nguvu ya kibinadamu au ya mkuu wa pepo. Hakuna nguvu ya chuki, hasira, maandamano, fujo, uharibifu, uchomaji vitu, vurugu, uuaji au roho za giza zinaweza kumshinda Shetani. Kwa sababu hivyo vyote ni vya Shetani, vyote hivyo ni nguvu ya Shetani.

Yesu alisema Shetani hawezi kumtoa Shetani. Hivyo tusitumie nguvu hizo za Shetani kumtoa Shetani aliyeiba haki za watanzania, bali tutumie Roho wa Mungu kumtoa Shetani. Hivyo maandamano hayawezi kutoa roho ya Shetani juu ya Tanzania. Ni nguvu za Mungu tu ndio zinaweza. Hivyo ndugu zangu msiende kupoteza maisha bure kwenye maandamano bila faida yeyote. Huu sio uoga nawapa, huu ni ukweli nawapa. Sikilizeni tafadhali nawaomba sana.

Tutumie mamlaka ya kiti cha enzi cha Roho ya Yesu Kristo, mamlaka ya jina la Yesu kumtoa Shetani kwa njia ya maombi. Tutumie upendo wa Roho, utii kwa Roho, unyenyekevu kwa Roho, utakatifu wa Roho, mamlaka ya Roho, nguvu za Roho, na silaha zingine zote za Mungu. Kwa njia hiyo tu pekee ndio tutapata ushindi. Mungu atusaidie sana kuelewa. Amina!!

07/02/2026

KANISA LIKIJINYENYEKEZA MBELE ZA MUNGU NDIPO TAIFA LA TANZANIA LITAPONYWA

Wito kwa Kanisa la Tanzania Kutubu, Kuomba, na Kuirejesha Nchi Kupitia Nguvu ya Agano la Mungu

NENO: (2 Mambo ya Nyakati 7:13–20)

Kilio cha Kanisa kwa Taifa Lililo Katika Mgogoro

Wapendwa, tunapoona mbingu kuonekana k**a zimefungwa katika Taifa, nchi kuonekana k**a kavu, na mioyo ya watu kuonekana k**a imepoa, ufisadi kuonekana k**a kuongezeka, damu isiyo na hatia kumwagika sana, na ukweli kuonekana k**a kutoweka nchini - hiyo si hali ya mgogoro wa kisiasa tu; bali hiyo ni hali ya mgogoro wa kiroho.

Mungu alisema katika (2 Mambo ya Nyakati 7:13–14),

“Nitakapozifunga mbingu ili mvua isiwepo, au kuamuru nzige kula nchi, au kutuma tauni kati ya watu wangu, ikiwa WATU WANGU WALIOITWA KWA JINA LANGU watajinyenyekesha, na kuomba na kunitafuta uso, na kugeuka kutoka njia zao mbaya, basi nitasikia kutoka mbinguni, nami nitawasamehe dhambi zao na kuiponya nchi yao.”

Neno hili halielekezwi kwa serikali, bali kwa watu wa Mungu — Kanisa.

K**a kuna ukavu katika nchi, si kwa sababu wanasiasa walishindwa, bali ni kwa sababu Kanisa liliacha kusimama katika nafasi yake ya kiroho na kuomba. Kanisa linapotubu, taifa hupona. Kanisa linapoomba, mbingu hufunguka tena.

Hoja ya 1: Mungu Anapofunga Mbingu, Anaita Toba ya Kanisa(mstari wa 13)

“Ninapofunga mbingu ili mvua isinyeshe…”

Wakati mwingine, Mungu huruhusu shida, ukame, au machafuko kutokea si kwa lengo la kutuangamiza bali kwa lengo la kutuvuta kwake.

Nchini Tanzania, tunapoona umwagaji damu, mgawanyiko, umaskini, na dhuluma, haya si matukio yanayotokea bila sababu; haya ni ishara za kiroho — ni ishara ya Mungu kuwaita watu wake waamke, watubu, waombe.

Fikiria baba akifunga mlango ili watoto wake waache kukimbia katika hatari na kusikiliza sauti yake. Vilevile, Mungu wakati mwingine hufunga mbingu hadi watoto wake warudi katika Neno Lake.

Hivyo kabla hatujawalaumu viongozi au watu wengine, ni lazima tujiangalie sisi wenyewe Kanisa kwanza. Je, tulijinyenyekeza kwa Roho Mtakatifu? Je, tuliutafuta kwa bidii uso wa Bwana? Je, tumetembea katika utakatifu? Je, tumeruhusu dhambi Kanisani? Je, tumeomba kwa ajili ya taifa au tumelalamika tu kuhusu hilo?

Hoja ya 2: Uponyaji wa Taifa Huanza na Kunyenyekea kwa Kanisa (mstari wa 14a)

“Ikiwa watu wangu, wanaoitwa kwa jina langu, watajinyenyekeza…”

Uponyaji wa nchi hauanzii katika jumba la kifalme — huanza katika chumba cha maombi. Hauanzii Bungeni — huanza katika madhabahu ya Kanisa.

Unyenyekevu unamaanisha kukubali kwamba hatuwezi kurekebisha Tanzania bila Mungu. Inamaanisha kuinama mbele ya Mfalme wa wafalme (Mungu) na kusema, “Bwana, tumetenda dhambi, utusamehe, na utuokoe na yule mwovu”

Mfano: Wakati Ninawi ilipojinyenyekeza chini ya ujumbe wa Yona, Mungu alibadilisha hukumu yake. Wakati watu wa Israeli walipofunga na kutubu chini ya Nehemia, Yerusalemu ilijengwa upya.

Ikiwa Mungu alifanya hivyo kwa ajili yao, anaweza kuifanya tena — kwa ajili ya Tanzania!

Lazima tuache kunyooshea vidole serikali au wengine, bali tuanze kupiga magoti mbele ya Mungu. Uamsho hauanzi kwa kiburi; huanza kwa kujinyenyekeza na kuomba toba kwa ajili yetu sisi wenyewe na wengine pia.

Hoja ya 3: Maombi na Kutafuta Uso wa Mungu Huleta Urejesho (mstari wa 14b)

“…na kuomba na kutafuta uso wangu…”

Kutafuta uso wa Mungu kunamaanisha kutafuta uwepo wake uwepo. Kutafuta Mungu mwenyewe awepo, na si kutafuta baraka zake tu ziwepo, bali kutafuta uwepo wake uwepo. Wengi wanataka uponyaji wa nchi bila uwepo wa Bwana, lakini uponyaji wa kweli wa taifa huja tu wakati Mungu mwenyewe unaporudi na kuwepo katika nchi.

Sanduku la Agano lilipoingia Yerusalemu wakati wa Daudi, taifa lilifurahi, na amani ikaijaza nchi. Uwepo wa Mungu unaporejeshwa katika Kanisa, taifa zima huhisi hivyo — amani, ustawi, na haki hufuata.

Kila Kanisa, kila mwamini lazima awe madhabahu ya maombi. Tanzania haitaponywa kwa mikakati, bali kwa moto wa maombezi unaoinuka kutoka kwa watu wa Mungu.

Hoja ya 4: Kugeuka Kutoka katika Njia Mbaya Hurejesha Neema ya Mungu (mstari wa 14c)

“…na kugeuka kutoka katika njia zao mbaya…”

Hii ndiyo ufunguo! Haitoshi kuomba — lazima tutubu kwa kugeuka.

Toba si kulia machozi; ni kugeuka na kubadilisha jinsi tunavyoishi. Inamaanisha kugeuka kutoka katika ufisadi, uasherati, chuki ya kikabila, umwagaji damu, ibada ya sanamu, na unafiki.

Mfalme Hezekia alipoharibu sanamu na kufungua tena hekalu, Mungu aliwapa Yuda ushindi dhidi ya maadui zao. Kanisa la Tanzania litakapoharibu sanamu za hasira, uchoyo, hofu, chuki, miungu, kutokusamehe, kutokuachilia, na kutokuelewana, Mungu atarejesha neema Yake kwa taifa.

Kila mchungaji, mtumishi wa Mungu, familia, na mwamini achunguze mioyo yao. Tusafishe madhabahu ya Mungu katika nyumba zetu na makanisa yetu. Tunapogeuka, mbingu pia zitageuka.

Hoja ya 5: Jibu la Mungu — Msamaha, Uponyaji, na Urejesho (mstari wa 14d–20)

“Ndipo nitasikia kutoka mbinguni, nitawasamehe dhambi zao, na kuiponya nchi yao.”

Mungu anaposamehe, laana huvunjwa. Anapoponya, nchi hustawi tena.

Haki inarudi, upendo unarudi, amani inarudi, baraka zinarudi, utawala bora unarudi. Haki itatiririka tena k**a mto.

Mungu pia anaahidi katika mistari ya 15–16:

“Macho yangu yatafunguliwa na masikio yangu yatasikiliza maombi yanayofanywa mahali hapa…”

Kanisa likifanya hayo, anasema macho yake yatakuwa juu ya Tanzania, na masikio yake yatasikia kilio cha watu wake.

NENO LA ONYO KWA KANISA LA TANZANIA

Mungu alimwambia Sulemani katika mstari wa 19:

“Lakini mkigeuka na kuziacha amri Zangu… nitawang’oa kutoka katika nchi Yangu.”

Hili ni onyo — si kwa Israeli tu bali kwa kila taifa linaloitwa kwa jina la Mungu.

Kanisa nchini Tanzania likiacha haki, nchi itaendelea kuteseka. Lakini ikiwa Kanisa litasimama katika utakatifu na maombi, Mungu atasimama na Tanzania.

Hitimisho: Kanisa Linashikilia Uponyaji wa Taifa

Hatima ya Tanzania haiko mikononi mwa wanasiasa, bali mikononi mwa Kanisa linaloomba. Kanisa linapotubu, taifa hufufuka. Kanisa linapoomba, mbingu hufunguka. Kanisa linapotembea katika haki, nchi hupona.

Wito wa Madhabahu: Wito kwa Kanisa kwa ajili ya Toba ya Taifa

Leo, Mungu anawaita watu wake — wachungaji, viongozi, waombezi, vijana — madhabahuni. Sio toba ya SERIKALI ambayo Mungu anaisubiri; bali ni toba yetu sisi KANISA.

Kila mwamini afanye MAOMBI kwa Mungu kuanzia leo mpaka tar 8/7. Kila Kanisa liwe nyumba ya sala tena. Kanisa lipige magoti mbele ya Mfalme wa utukufu — naye ataiponya nchi yetu.

Tamko la Mwisho:

“Tanzania itainuka tena, si kwa siasa, bali kwa nguvu ya Roho Mtakatifu iliyo katika Kanisa.”

K**a Kanisa litasimama katika nafasi yake, nchi ya Tanzania itapona. Kanisa lisiposimama nchi inaweza isipone.

06/30/2026

GOD HAS DECLARED OUR END WITH GOD’S GREAT GLORY FROM BEGINNING

“I am God, and there is none else; I am God, and there is none like me, declaring the END from the BEGINNING, and from ancient times the things that are not yet done, saying, My counsel shall stand, and I will do all my pleasure” (Isaiah 46:9-10).

God in (Genesis 1:26) has declared our END with great God’s glory from the BEGINNING, when he said, “Let us make man in our IMAGE, after our LIKENESS; and let them have DOMINION over the fish of the sea, and over the fowl of the air, and over the cattle, and over all the earth, and over every creeping thing that creepeth upon the earth.”

There are three (3) things God has declared that will happen to us in these END days from the BEGINNING. Those are;

1. The IMAGE of God
2. The LIKENESS of God
3. The AUTHORITY of God to rule the whole world.

That is God's purpose for us in these END days. He came through Jesus in these LAST days to fulfill his purpose to MAN as He planned from beginning, after it failed from the first Adam.

Jesus came to save us and make us children of God again through His Spirit, so that we can again have the IMAGE of God, and have a life LIKE God, and also give us the AUTHORITY OF THE NAME OF JESUS ​​so that we can rule again over all things on the earth.

"You have put off the old self with its practices; and have put on the new self, which is being renewed in knowledge according to the IMAGE of Him who created it" (Colossians 3:9-10).

“Put off, concerning your former conduct, the old self, which is being corrupted according to the deceitful lusts; and be renewed in the spirit of your mind; and put on the new self, which was created after the LIKENESS of God in righteousness and true holiness” (Ephesians 4:22-24).

“Behold, I have given you AUTHORITY to tread on serpents and scorpions, and over all the power of the enemy; and nothing shall by any means hurt you. Nevertheless, do not rejoice that the spirits are subject to you; but rejoice that your names are written in heaven” (Luke 10:19-20).

“And these signs shall follow them that believe; In [the AUTHORITY OF] MY NAME they shall cast out devils; they shall speak with new tongues; they shall take up serpents; and if they drink any deadly thing, it shall not hurt them; they shall lay hands on the sick, and they shall recover” (Mark 16:17-18).

These are the three things that Jesus came to restore to us all, as He intended us to have in these last days from the beginning. So again those are;

* THE IMAGE OF GOD = THE SPIRIT OF GOD

* THE LIKENESS OF GOD = A LIFE (CHARACTER) LIKE GOD
* THE AUTHORITY OF GOD = THE AUTHORITY OF THE POWER OF GOD'S GOVERNMENT.

Each of us should have those three things again in these last days.

06/30/2026

MUNGU ALISHATANGAZA MWISHO WETU WENYE UTUKUFU MKUU WA MUNGU TOKA MWANZO WETU

“Mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye k**a mimi; nitangazaye MWISHO tangu MWANZO, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote” (Isaya 46:9-10).

Mungu katika (Mwanzo 1:26) alishatangaza MWISHO wetu toka MWANZO, aliposema, “Na tumfanye mtu kwa SURA yetu, kwa MFANO wetu; WAKATAWALE samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.”

Kuna vitu vitatu (3) Mungu alishavitangaza vitakavyokuwa kwetu katika siku hizi za MWISHO toka MWANZO. Navyo ni;

1. Sisi kuwa na SURA ya Mungu
2. Sisi kuwa na MFANO wa Mungu
3. Sisi kuwa na MAMLAKA ya kutawala ulimwengu wote.

Hilo ndilo kusudi la Mungu kwetu alilokuja kulitimiza kwetu katika siku hizi za MWISHO kupitia Yesu Kristo, baada ya kufeli kwa Adamu wa kwanza.

Yesu alikuja kutuokoa na kutufanya tena kuwa wana wa Mungu kwa njia ya Roho wake, ili nasi tena tuweze kuwa na SURA ya Mungu, na kuwa na maisha ya MFANO wa Mungu, na pia kutupatia tena MAMLAKA YA JINA LA YESU ili tuweze tena kutawala vitu vyote ulimwenguni.

“Mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake; mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na SURA yake yeye aliyeuumba” (Wakolosai 3:9-10).

“Mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya; na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa MFANO wa Mungu katika haki na utakatifu wa kweli” (Waefeso 4:22-24).

“Tazama, nimewapa MAMLAKA ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni” (Luka 10:19-20).

“Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa [MAMLAKA YA] JINA LANGU watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya” (Marko 16:17-18).

Hivyo vitu vitatu ndio Yesu alikuja kutupatia au kuturejeshea sisi sote k**a alivyokusudia tuwe navyo katika siku hizi za mwisho toka mwanzo. Hivyo tena ni;

* SURA YA MUNGU = ROHO YA MUNGU
* MFANO WA MUNGU = MAISHA (TABIA) K**A YA MUNGU
* MAMLAKA YA MUNGU = MAMLAKA YA NGUVU YA UTAWALA YA MUNGU.

Kila mmoja wetu tunapaswa kuwa na hivyo vitu vitatu tena katika siku hizi za mwisho.

06/17/2026

MAISHA YA UMOJA WA KANISA NDIO MAISHA YANAYOMDHIHIRISHA MUNGU

“Sikiza, Ee Israeli; BWANA, Mungu wetu, BWANA ndiye mmoja” (Kumbukumbu 6:4).

K**a Mungu ni mmoja, maana yake maisha yake ni ya umoja. Hivyo Kanisa kupewa maisha ya ki-Mungu ni kupewa maisha ya umoja, maana Mungu ni mmoja na maisha yake ni ya umoja.

Maisha ya umoja wa Mungu ndio maisha ya mbinguni tuliyopewa tuyadhihirishe duniani. Kwa sababu duniani hakuna maisha ya umoja wa Mungu kwa sababu ya chuki iliyopo duniani.

Upendo wa Mungu, ndio upendo uliotuunganisha sisi tena na Mungu na kutufanya kuwa Roho moja naye, na ndio pia uliotuunganisha sisi sote tena katika Kristo na kutufanya kuwa MWILI au HEKALU MOJA la Roho wa Mungu.

Maisha ya chuki ya duniani yanatenganisha watu, bali maisha ya upendo ya mbinguni yanaunganisha watu pamoja. Maisha ya chuki ya duniani yanatenganisha kanisa, bali maisha ya upendo ya mbinguni yanaunganisha kanisa pamoja. Maisha ya chuki katika kanisa yanamtukuza SHETANI, bali maisha ya upendo katika kanisa yanamdhihirisha YESU.

Ndugu zangu tuyakatae kabisa maisha ya chuki ndani ya kanisa yanayotutenganisha na kumdhihirisha Shetani badala ya kumdhihirisha Yesu. Mungu atusaidie sana kanisa lake tumdhihirishe Yesu na sio Shetani, kwa kukaa pamoja na kwa umoja. Amina!!

Address

Willmar, MN

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when The Kingdom of Heaven posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share